Posts

Showing posts from April, 2023

Nini Fadhila Za Sitta Shawwaal?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Swiyaam za Siku Sita Za Shawwaal baada ya Swiyaam za Ramadhwaan ni kama Swiyaam ya mwaka." [Al-Fataawaa (20/17)]

Je, Swiyaam Za Sitta Shawwaal Zinapaswa Kwa Wanaume Na Wanawake?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Ni kwa wanaume na wanawake." [Al-Fataawaa 20/17)]

Swiyaam Za Sita Shawwaal Ni Lazima Kuanza Baada Tu Ya 'Iydul-Fitwr?

Image
Swiyaam Za Sita Shawwaal Ni Lazima Kuanza Baada Tu Ya EiIydul-Fitwr? SWALI : Je, swiyaam za Sitta Shawwaal ni lazima kuanza kufunga siku ya pili tu baada ya 'Iydul-Fitwr au inaruhusiwa kuanza baada ya siku chache?       JIBU : Si lazima kwa mtu kuanza Swiyaam baada ya siku ya kwanza ya 'Iyd, bali anaweza kuanza siku ya pili au ya tatu au hata zaidi ya masiku ndani ya mwezi huo wa Shawwaal. Vile vile anaweza kufunga moja kwa moja bila ya kusita au kufunga na kupumzika kwani jambo hili ni dhahiri kuwa si fardhi bali ni Sunnah. [Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil Buhuwth Al-‘Ilmiyyaa Wal Iftaa Fatwa 3475  – Fataawaa Ramadhwaan – Majalada 2, Ukurasa 693, Fatwa Namba 698] EID MUBAARAQ

Kulipa Ramadhwaan Au Siku Sita Za Shawwaal? Inafaa Kulipa Jumatatu Na Alkhamiys?

Image
SWALI: Je, inafaa kufunga siku sita za Shawwaal kabla ya kulipa deni la Ramadhwaan? Na inaruhusiwa kulipa kwa kufunga siku za Jumatatu na Alkhamiys katika mwezi wa Shawwaal kwa niyyah ya kulipa deni na niyyah ya kupata thawabu za Swiyaam za Sunnah ya Jumatatu na Alkhamiys? JIBU : Thawabu za kufunga Sittatu Ash-Shawwaal hazipatikani ila baada ya kukamilisha mwezi wa Ramadhwaan. Kwa hiyo kama mtu ana deni la Ramadhawan basi kwanza alipe deni kisha ndio afunge Siku Sita Za Shawwaal, kwani Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: مَنْ صَامَ رَمَضَانَ ثُمَّ أَتْبَعَهُ سِتًّا مِنْ شَوَّالٍ كَانَ كَصِيَامِ الدَّهْرِ   ((Atakayefunga Ramadhwaan, kisha akafuatia na Sitta za Shawwaal Swiyaam zake zitakuwa kama ni Swiyaam za mwaka)) [Muslim, Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad, Ad-Daarimiy]. Kutokana na Hadiyth  hiyo tunasema kwamba, yeyote mwenye deni la Swawm ya Ramadhwaan alipe kwanza kisha ndio afunge Siku Sita Za Shawwaal. Na ikiwa Siku Sita za Shaw...

Swiyaam Za Siku Za Sita Za Shawwaal, Je, Ni Lazima Mtu Kufunga Kila Mwaka?

Image
SWALI : Ikiwa mtu alikuwa akifunga Sitta Shawwaal, kisha akaumwa au hakuweza kufunga kwa sababu aliona ngumu kufunga mwaka mmoja. Je, ni dhambi kwake kuacha Swiyaam hizo? Kwa sababu amesikia kwamba anayeanza kufunga Swiyaam za Sitta Shawwaal inakuwa ni lazima aendeleze kila mwaka  na akiacha ni dhambi kwake. Je, ni kweli? JIBU : Swiyaam za Siku Sita Za Shawwaal baada ya 'Iydul-Fitwr ni Sunnah. Hivyo si fardhi kwa anayefunga mwaka mmoja au zaidi (Akiweza anafunga na asipoweza anaacha kufunga) Na si dhambi kwa anayeacha kufunga. [Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil-Buhuwth Al-‘Ilmiyyah Wal Iftaa Fatwa Namba 7306 -  Fataawaa Ramadhwaan – Mjalada 2, ukurasa 696, Fatwa namba 702]

Swawm Ya Siku Sita Za Shawwaal Zikiangukia Jumatatu Na Alkhamiys Kunapatikana Thawabu Kwa Zote Ikiwekwa Niyyah Mbili

Image
Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Inapoafikiana kuwa Swawm katika masiku haya sita (siku sita za mwezi wa Shawwaal) na (yakukutana) na siku ya Jumatatu au Alkhamiys, basi (mtu) hupata ujira wa (Swawm) mbili (anapofunga) kwa niyyah  ya (kupata) ujira wa masiku sita (ya Shawwaal) na kwa niyyah ya (kupata) ujira wa siku ya Jumatatu au Alkhamiys, kwa kauli yake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika matendo (hulipwa) kwa niyyah, na hakika kila mtu (hulipwa) kwa kile alichonuia." [Fataawaa Islaamiyyah, mj. 2, uk. 154]

Je, Mwenye Deni La Ramadhwaan Atapata Thawabu Akifunga Sitta Shawwaal Kabla Kulipa Deni Lake?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Ni waajib kukimbilia kulipa deni hata kama Sitta Shawwaal zitampita kutokana na Hadiyth iliyotajwa na kwa sababu fardhi inatangulizwa kabla ya naafil (Sunnah)." [Al-Fataawaa (15/393)] Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: Hawezi mtu kupata thawabu za Swiyaam za Sitta Shawwaal isipokuwa ikiwa amemaliza Swiyaam za mwezi wa Ramadhwaan. [Al-Fataawaa (18/20)]

Vipi Kuzifunga Swiyaam Za Sitta Shawwaal?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Muumini huchagua atakavo kuzifunga katika mwezi wote; akitaka afunge mwanzo wake, au katikati yake au mwishoni mwake, na akitaka afunge kwa kutofululiza, na akitaka afululize." [Al-Fataawaa (15/390)]

Lipi Lililo Bora Katika Kufunga Sitta Shawwaal?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Akifanya hima kuzifunga mwanzoni mwa mwezi basi ni bora zaidi." [Al-Fataawaa (15/390)] Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Lililo bora kufanywa kuhusu Swiyaam za Sitta Shawwaal ni kuzifunga siku sita baada ya ‘Iyd na ziwe za kufufuliza." [Al-Fataawaa (20/20)]

Je, Swiyaam Za Sitta Shawwaal Zinapaswa Kufungwa Mfulululizo?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Inajuzu kuzifunga mfululizo au kutokufululiza." [Al-Fataawaa 15/391)]

Je, Akifunga Sitta Shawwaal Atawajibika Kufunga Kila Mwaka?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Akifunga baadhi ya miaka na akaacha baadhi ya miaka hakuna ubaya kwa sababu hiyo ni Sunnah na si fardhi." [Al-Fataawaa (20/21]

Ni Lazima Kutia Niyyah Usiku Kwa Ajili Ya Swiyaam Za Sitta Shawwaal?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Hakuna budi kutia niyyah kabla Alfajiri ili apate kutimiza siku hiyo." [Al-Fataawaa (19/184)]

Vipi Kuhusu Wasemao Kuwa Swiyaam Ya Sitta Shawwaal Ni Bid’ah?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Kauli hii ni batili." [Al-Fataawaa (16/389)]

Je, Inafaa Kutanguliza Swiyyaam Za Sitta Shawwaal Kabla Ya Swiyaam Za Kafara?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Lililo waajib ni kuhimiza Swiyyaam za kafara wala haijuzu kutanguliza Swiyaam za Sitta Shawwaal kabla yake kwa sababu hizo ni Naafil (Sunnah) na kafara ni fardhi ambayo ni waajib ipasayo kutimizwa haraka." [Al-Fataawaa (15/394)]

Inafaa Kuunga Swiyaam Za Sitta Shawwaal Baada Ya Kumaliza Deni?

Image
Imaam Ibn Baaz  (Rahimahu Allaah) amesema: "Hakuna ubaya kufanya hivyo." [Al-Fataawaa (15/396)]

Je, Inajuzu Kufunga Sitta Za Shawwaal Katika Mwezi Wa Dhul-Qa’dah Ikiwa Na Deni La Mwezi Mzima?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Ikiwa mfano mtu alikuwa ana deni la mwezi mzima wa Ramadhwaan kwa sababu ya kuwa safarini, au kuuguwa au kutokana na kuzaa, kisha akafunga kulipa deni mwezi wa Shawwaal na ukamalizika mwezi wote kulipa tu, basi anaweza kufunga Swiyyaam za Sitta katika mwezi wa Dhul-Qa’dah...  Ama ikiwa amefanya upuuzi katika kulipa deni kisha siku zikampita asiweze kufunga deni la Ramadhwaan hadi ikafika mwisho wa Shawwaal kisha akataka kufuatilia Sitta za Shawwaal basi hii haijuzu kwake." [Liqaat Al-Baab Al-Maftuwh (117)]

Zipi Zinapaswa Kutangulizwa Swiyaam Za Nadhiri Au Za Sitta Shawwaal?

Image
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema: "Linalokupasa kwanza ni kufunga Swiyaam zilobakia za nadhiri kisha ndio ufunge Sitta za Shawwaal utakapoweza kwa sababu Swiyaam za Sitta Shawwaal ni mustahabb (Sunnah). Ama Swiyaam za nadhiri ni waajib. [Mawqi’ Shaykh bin Baaz]

Je, Inafaaa Swiyaam Za Sunnah Bila Ya Kutanguliza Niyyah?

Image
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Ikiwa mtu hakutia niyyah kufunga Swiyaam za Sitta Shawwaal isipokuwa akatia niyyah mchana, basi hatoandikiwa kuwa amefunga siku kamili. Basi akitia niyyah siku ya kwanza wakati wa Adhuhuri, kisha baada ya hapo akafunga siku tano, basi atakuwa hakuzipata siku sita kwa sababu amefunga siku tano na nusu, kwa vile thawabu haziandikwi isipokuwa kwa niyyah kutokana na kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Hakika kusihi kwa ‘amali huzingatiwa na niyyah. Na hakika kila mtu atalipwa kwa kile alichokinuia.” Na hivyo yeye mchana wa siku hiyo hakutia niyyah kufunga kwa hivyo hapati ukamilifu wake.  Naam." [Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb, kanda (296)

Nini Hikmah Ya Swiyaam Za Sitta Shawwaal?

Image
Nini Hikmah Ya Swiyaam Za Sitta Shawwaal? Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Hikmah yake ni kukamilisha fardhi, basi atakapofunga Swiyaam za Sitta Shawwaal ni kama vile Swalaah za Sunnah ambazo zinakuwa ni kukamilisha humo kilichopungua katika fardhi."  [Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb, kanda (75)]

Je, Mtu Akifunga Siku Tatu Au Tano Kwa Ajili Ya Sitta Shawwaal Atapata Thawabu?

Image
Je, Mtu Akifunga Siku Tatu Au Tano Kwa Ajili Ya Sitta Shawwaal Atapata Thawabu? Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Naam, atapata thawabu lakini hatopata thawabu ambazo ameziainisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika kauli yake: “Atakayefunga Ramadhwaan kisha akafuatiliza na Sitta Shawwaal itakuwa kama ni Swiyaam ya mwaka” [Muslim]."  [Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb, Kanda (75)]

Je, Inafaa Kujumuisha Niyyah Ya Sitta Shawwaal Na Swiyaam Za Jumatatu Na Alkhamiys?

Image
Je, Inafaa Kujumuisha Niyyah Ya Sitta Shawwaal Na Swiyaam Za Jumatatu Na Alkhamiys? Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Itakapowafikiana kuwa Swiyaam za Masiku ya Sitta Shawwaal yameangukia Jumatatu na Alkhamiys, basi atapata thawabu mbili kwa niyyah ya Swiyaam za Sitta Shawwaal pamoja na niyyah ya Jumatatu na Alkhamiys kutokana na kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Hakika kusihi kwa ‘amali huzingatiwa na niyyah. Na hakika kila mtu atalipwa kwa kile alichokinuia.”  [Al-Fataawaa (20/18-19)]

Je, Inafaa Kuzifanya Swiyaam Za Sitta Shawaal Kuwa Ni Kulipa Deni La Ramadhwaan?

Image
Je, Inafaa Kuzifanya Swiyaam Za Sitta Shawaal Kuwa Ni Kulipa Deni La Ramadhwaan? Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: "Swiyaam za Sitta Shawwaal hazifai kufanywa ni deni la Ramadhwaan kwa sababu siku sita hizo zinafutilia baada ya Ramadhwaan, zinafanana na Swalaah za Sunnah za Raatibah (zile Sunnah za Qabliyyah na Ba'diyyah) katika Swalaah za fardhi. [Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb (175)

Mlango Wa Rayyan Peponi Wataingia Wenye Swawm

Image
Mlango Wa Rayyan Peponi Wataingia Wenye Swawm عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ رضى الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( فِي الْجَنَّةِ ثَمَانِيَةُ أَبْوَابٍ، فِيهَا باب يُسَمَّى الرَّيَّانَ لاَ يَدْخُلُهُ إِلاَّ الصَّائِمُونَ ‏)) البخاري Imepokelewa toka kwa Sahl bin Sa’d (Radhwiya Allaahu 'anhu)  kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Peponi kuna milango minane. Humo kuna mlango uitwao Rayyaan, hawauingii isipokuwa Asw-Swaaimuwn (wafungaji)) [Al-Bukhaariy]   Mafunzo : Mlango huu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameuweka maalumu kwa ajili ya wafungaji (Swawm) tu. Wafungaji peke yao ndio watakaopita kwenye mlango huu. Umeitwa Rayyaan kutokana na wingi wa mito inayopita kuelekea kwake pamoja na maua na matunda mazuri yenye kuuzunguka. Pia umeitwa hivyo kwa kuwa mwenye kuufikia, kitamwondokea kiu kikali cha Siku ya Qiyaamah, na kisha atadumu milele na hali ya kutohisi kiu. Aidha, umeitwa hivi kwa kuwa ni jazaa kwa wafungaji kutokana na kiu ...

Swawm Hufuta Madhambi Yatokanayo Na Mtu Kufitinika Na Mkewe Na Mali Yake

Image
Swawm Hufuta Madhambi Yatokanayo Na Mtu Kufitinika Na Mkewe Na Mali Yake سأل عمر رضي الله عنه قال: من يحفظ حديثًا عن النبي صلى الله عليه وسلم في الفتنة؟  قال حذيفة: أنا سمعته يقول: ((فِتْنَةُ الرَّجُلِ فِي أَهْلِهِ وَمَالِهِ وَجَارِهِ تُكَفِّرُهَا الصَّلَاةُ وَالصِّيَامُ وَالصَّدَقَةُ)). ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu)  aliuliza: “Nani anahifadhi Hadiyth toka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu fitnah?” Hudhayfah akasema: Mimi nimemsikia akisema: ((Kufitinika mtu kutokana na mke wake, mali yake na jirani yake, (dhambi yake) hufutwa na Swalaah na Swawm na swadaqah..)) [Al-Bukhaariy] Mafunzo: Maana ya fitnah hapa ni makosa anayoyafanya mtu kutokana na mkewe na watoto kwa kujaribu kuwafurahisha kwa linalomkasirisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), au kuitumia mali yake visivyo akaipeleka kwenye sehemu isipo pake, au akakiuka haki za ujirani mwema kwa kumuudhi jirani yake kimatendo au kimaneno na kadhalika. Asili ya neno “fitnah” ni الابتلاء na الاختبار...

Du’aa Ya Mwenye Swawm Hairejeshwi

Image
Du’aa Ya Mwenye Swawm Hairejeshwi عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((ثَلاثَةٌ لا تُرَدُّ دَعْوَتُهُمْ الإِمَامُ الْعَادِلُ وَالصَّائِمُ حِينَ يُفْطِرُ وَدَعْوَةُ الْمَظْلُومِ ))  Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)  akisema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Watatu du’aa zao hazirejeshwi: Imaam (kiongozi)  mtenda haki, mwenye Swawm wakati anapofungua, na du’aa ya aliyedhulumiwa)) [Imesimuliwa na At-Tirmidhiy Hadiyth nambari (2525), na Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh katika Swahihy At-Tirmidhiy Hadiyth nambari (2050)]   Mafunzo : Hadiyth hii tukufu ni dalili ya kuwa mwenye Swawm anatakiwa akitumie kitambo cha wakati wa kufungua Swawm yake kwa kuomba du’aa ya kheri, kwani wakati huo du’aa hujibiwa. Bora zaidi cha kusema wakati huo ni yale yaliyopokelewa na ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) aliyesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam...

Swawm Na Qur-aan Zitamuombea Mja Ash-Shafaa’ah Siku Ya Qiyaamah

Image
Swawm Na Qur-aan Zitamuombea Mja Ash-Shafaa’ah Siku Ya Qiyaamah وعَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ : ((الصِّيَامُ وَالْقُرْآنُ يَشْفَعَانِ لِلْعَبْدِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ يَقُولُ الصِّيَامُ أَيْ رَبِّ مَنَعْتُهُ الطَّعَامَ وَالشَّهَوَاتِ بِالنَّهَارِ فَشَفِّعْنِي فِيهِ وَيَقُولُ الْقُرْآنُ مَنَعْتُهُ النَّوْمَ بِاللَّيْلِ فَشَفِّعْنِي فِيهِ قَالَ فَيُشَفَّعَانِ))   Imepokelewa toka kwa Abdullaah bin ‘Amr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swiyaam na Qur-aan zitamwombea shafaa’ah (uombezi) mja Siku ya Qiyaamah. Swawm itasema: “Nilimzuia chakula na matamanio yake mchana, basi Niwezeshe nimwombee shafaa’ah. Na Qur-aan itasema: Nilimzuia usingizi usiku, basi Niwezeshe nimwombee shafaa’ah. Akasema, basi vitaomba shafaa’ah)) [Ahmad ni Hadiyth Swahiyh taz Swahiyh Al-Jaami’ (3882)] Mafunzo : Mwenye Swawm anatakiwa akithirishe kusoma Qur-aan Tukufu katika ma...

Sita Za Shawwaal Na Swawm Nyinginezo Baada Ya Ramadhwaan

Image
Sita Za Shawwaal Na Swawm Nyinginezo Baada Ya Ramadhwaan Ndugu Waislam, baada ya kuuaga mwezi mtukufu wa Ramadhwaan, ambao umejaa fadhila nyingi na kheri zisizopatikana katika miezi kumi na moja iliyobaki, kuna umuhimu mkubwa wa kuendeleza zoezi hili la Funga baada ya mwezi huu mtukufu hususan, na kwa mwaka mzima kwa ujumla In shaa Allaah. Swawm kwa ujumla na Swawm za Sunnah haswa ni jambo kubwa sana la ki-'Ibaadah. Na ni bora sana ieleweke ndugu zangu, kuwa Swawm si 'Ibaadah ifanyikayo katika mwezi wa Ramadhwaan pekee, bali ni jambo ambalo linalofanyika mwaka mzima katika nyakati mbalimbali kama tutakavyoona katika makala haya.  Kama ilivyo katika ‘Ibaadah ya Swalah, kuna Swalah za Sunnah au Rawaatib au Nawaafil, ambazo ndizo zitakazokuwa viraka siku ya Qiyaamah wakati zile Swalah za Fardh zitakapopelea katika Mizani. Nazo Swawm za kujitolea au za Sunnah, ndizo zitakazomuongezea mja thawabu na ujira pamoja na ile Swawm yake ya Fardh ambayo ni Ramadhwaan. Hapa chini tutaziorodh...

Fadhila Za Laylatul-Qadr

Image
Fadhila Za Laylatul-Qadr عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((مَن قام ليلةَ القدر إيمانًا واحتسابًا، غُفر له ما تقدَّم من ذنبه)) متفق عليه. Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)   kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Mwenye kusimama Usiku wa Laylatul-Qadr kwa iymaan na kutaraji malipo, hughufiriwa madhambi yake yaliyotangulia)) [Al-Bukhaariy, Muslim] Mafunzo : Hadiyth hii ina faida kadhaa: 1-Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameutunuku umma wetu huu usiku huu wa barka wenye sifa hizi mahsusi: 2-Ni usiku uliobarikiwa kwa kheri zake nyingi, fadhila na thawabu kochokocho. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)   Anasema: إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ﴿٣﴾  Hakika Sisi Tumeiteremsha (Qur-aan) katika usiku uliobarikiwa [Ad-Dukhaan: 3] 3-Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameteremsha ndani yake Qur-aan Tukufu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa ...

Sifa Za Laylatul-Qadr

Image
Sifa Za Laylatul-Qadr عَنْ أَبِي هُرَيْرَة رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : لَمَّا حَضَرَ رَمَضَان قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  ((قَدْ جَاءَكُمْ شَهْرُ رَمَضَان شَهْرٌ مُبَارَكٌ اِفْتَرَضَ اللَّهُ عَلَيْكُمْ صِيَامَهُ تُفْتَح فِيهِ أَبْوَاب الْجَنَّة وَتُغْلَق فِيهِ أَبْوَابُ الْجَحِيم وَتُغَلُّ فِيهِ الشَّيَاطِين فِيهِ لَيْلَة خَيْرٌ مِنْ أَلْف شَهْر مَنْ حَرُمَ خَيْرهَا فَقَدْ حُرِمَ)) وَرَوَاهُ النَّسَائِيّ Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraryah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba ilipofika Ramadhwaan, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Umekujieni mwezi wa Ramadhwaan, ni mwezi wa Baraka.  Imefanywa Swawm kwenu kuwa ni fardhi, milango ya Jannah hufunguliwa na milango ya moto hufungwa na mashaytwaan hufungwa. Katika mwezi huu, kuna usiku ulio bora kuliko miezi elfu.  Atakayenyimwa kheri zake, basi hakika amenyimwa!)) [An-Nasaaiy] Mafunzo : Ni vipi Mwislamu ataujua usiku huo? Kuna baadhi ya alama zilizothibitishwa na Ha...