Posts

Showing posts from January, 2024

MANABII NA MITUME WA ALLAH

Image
MANABII NA MITUME WA ALLAH Assalam Alykum Warahmatullah Wabarakat. Pamoja na kwamba inasemwa kuwa idadi ya Manabii wanafika hadi 124,000 kutokana na baadhi ya mapokezi, lakini Hadiyth hizo zimedhoofishwa na hivyo hatuwezi kuzitegemea, ila kuna Hadiyth ambayo Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) iliyosimuliwa na Abu Dhar ambayo alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) idadi ya Manabii (‘Alayhim wa sallam) na akamjibu kuwa ni mia tatu na makumi kadhaa. Hadiyth hiyo imeelezwa usahihi wake na Imaam Al-Albaaniy kama ilivyo hapa chini: عن أبي ذر ، قال : قلت : يا رسول الله ! أي الأنبياء كان أول ؟ ! قال : آدم ، قلت : يا رسول الله ! ونبي كان ؟ ! قال : نعم نبي مكلم ، قلت : يا رسول الله : كم المرسلون ؟ ! قال : ثلاث مئة وبضعة عشر ؛ جما غفيرا . الراوي: أبو ذر الغفاري  -  خلاصة الدرجة: صحيح  -  المحدث: الألباني  -  المصدر: مشكاة المصابيح  -  الصفحة أو الرقم: 566 Kutoka kwa Abu Dhar ambaye amesema: Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah...

SIYRAH YA MTUME MUHAMMAD S.A.W

Image
SIYRAH YA MTUME MUHAMMAD S.A.W KUZALIWA KWA MTUME Bwana Mtume – Allah amshushie rehma na amani – alizaliwa katika mji wa Makkah, siku ya Jumatatu mwezi wa mfungo sita, mwaka wa tembo sawa na tarehe 20 ya mwezi April mwaka 571 – Miyladia (tangu kuzaliwa Nabii Issa). Bwana Mtume alizaliwa hali ya kuwa ni yatima kwani baba yake alikufa akimuacha mkewe ana mimba ya Mtume. Mama yake alipojifungua tu alimpeleka mjumbe kwa babu yake Mtume Mzee Abdul -Mutwalib kumpa khabari njema za kuzaliwa mjukuu wake. Mzee Abdul – Mutwalib akafurahikia sana mjukuu wake akamchukua na kumzungusha katika Al-Kaaba na akamuita Muhammad. Tumesema Bwana Mtume amezaliwa mwaka wa tembo. Qur-ani Tukufu imeuzungumza mwaka huu katika sura maalum iliyoitwa kwa jina la Suuratul –Fiyl (Sura ya tembo). Kisa cha mwaka wa tembo kinaanzia pale Abraha mfalme wa Habashah na Yaman alipowaona Waarabu wakihiji Makkah na ibada hii ya Hijjah ikaufanya mji wa Makkah kuwa ni kitovu cha biashara . Mfalme Abraha akadhamiria kuihamisha i...

SIRA YA NABII ISSA (A.S)

Image
SIRA YA NABII ISSA (A.S) Disemba 25 ni siku inayosadifiana na kumbukumbuu ya kuzaliwa Nabii Issa Masiya mwana wa Maryamu (Alayhas salaam) kwa mujibu wa imani ya Wakristo wengi. Mtume huyo mwema alikuwa mtoa bishara njema na mlinganiaji wa kweli na upendo na itikadi na Mungu Mmoja. Isa Masiih alizungumza kwa amri ya Allaah akiwa katika susu na kuwaambia watu waliokuwa katika mghafala wa zama hizo kama inavyotwambia aya ya 30 hadi 33 za Surat Maryam kwamba:  قَالَ إِنِّي عَبْدُ اللَّهِ آتَانِيَ الْكِتَابَ وَجَعَلَنِي نَبِيًّا وَجَعَلَنِي مُبَارَكًا أَيْنَ مَا كُنتُ وَأَوْصَانِي بِالصَّلاةِ وَالزَّكَاةِ مَا دُمْتُ حَيًّا وَبَرًّا بِوَالِدَتِي وَلَمْ يَجْعَلْنِي جَبَّارًا شَقِيًّا وَالسَّلامُ عَلَيَّ يَوْمَ وُلِدتُّ وَيَوْمَ أَمُوتُ وَيَوْمَ أُبْعَثُ حَيًّا “Na akasema: Hakika mimi ni mja wa Allaah, amenipa kitabu na kunifanya Nabii. Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo na ameniusia Swala na Zaka maadamu ni hai. Na kumtendea wema mama yangu. Wala hakunifanya jeuri, mu...

ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)

Image
 ZAKARIA(A.S)  NA  YAHYA(A.S) Nabii Zakaria(a.s) ni miongoni mwa mitume wa Bani Israil (Mayahud) na anatokana na kizazi cha Nabii Sulaiman(a.s).  Alikuwa mwangalizi mkuu wa nyumba ya Ibada na alikuwa anapta riziki yake kwa kazi ya useremala. Zakaria(a.s)  Kumlea  Maryam  na  Kuomba  Mtoto Mwema Zakaria(a.s) alichaguliwa  na ukoo kumlea Maryamu, mama yake Nabii Issa(a.s).   Alimlea vyema  katika malezi ya kiislamu. Katika kumlea Marymu, Zakaria(a.s) siku moja alishangaa kumkuta Maryam binti Imraan na vyakula mezani ambavyo hakumpa yeye, ikabidi amuulize: “... Ewe Maryam! unapta wapi hivi ?  Akasema: Hivi vinatoka kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu” (3:37)  Jibu hili la Maryamu lilimsisimua na kumuhamasisha Mzee Zakaria kiasi cha kumfanya naye amuelekee Mola wake na kumuomba mtoto mwema atakaye mrithi katika ucha-mungu na kusimamisha Dini ya  Allah(s.w) katika jamii. ...

SIRA YA NABII YUNUS

Image
SIRA YA NABII YUNUS Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemtaja Yunus kuwa ni katika Mitume na katika watu wema. Vile vile amemwita kwa jina sahiba wa samaki. Pia akamwita mwenye kughadhibika. Kwa sababu aliwalingania watu wake kwenye imani, lakini hawakumwitikia ndipo akawaombea maangamizo na akawaondokea kwa kukata tamaa na imani yao. Katika Sura Al-Qalam Mwenyezi Mungu amemwamrisha Mtume wake Muhammad (s.a.w.), avumilie na asifanye haraka ya kuwaombea adhabu watu wake, kama alivyofanya Yunus. فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُنْ كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ {48} “Basi subiri hukumu ya Mola wako, wala usiwe kama sahiba wa samaki, aliponadi na hali amezongwa.” (68:48). Watu wa Yunus walikuwa kiasi cha laki moja (100,000). Mwenyezi Mungu anasema: وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ {147} “Na tulimtua kwa watu elfu mia moja au zaidi.” (37:147). Wapokezi na wafasiri wanasema kuwa watu wa Yunus walikuwa wakikaa katika ardhi ya Mousel, na kwamba wao walikuwa w...

NABII ILYAAS

Image
NABII ILYAAS Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Alitumwa kwa watu ambao walitupa mafundisho ya Mitume waliotangulia na badala yake wakawa wanaabudu Mungu- jua waliyemuita - Baal. Mtume Ilyasa(a.s) aliwaita watu wake wamwabudu Mungu Mmoja, Allah(s.w); lakini walimkadhibisha. Kwa ajili hiyo ya kukataa mafundisho ya Mtume wao, wakawa katika kundi la watakaoingia katika adhabu ya Allah(s.w). Isipokuwa kwa wale waliorejea kwa Mola wao wakajitakasa. Kwa muhtasari ujumbe wa Mtume Ilyasa(a.s) unapatikana katika aya zifuatazo: " Na hakika Ilyas alikuwa miongoni mwa Mitume. (Wakumbushe) Alipowaambia watu wake: "Oh! Hamuogopi?" "Mnamuomba (na kumuabudu) Baal na mnamuacha aliye Mbora wa waumbaji (na ndiye Muumbaji peke yake). " "Mwenyezi Mungu, Mola wenu na Mola wa wazee wenu wa mwanzo!" Wakamkadhibisha. Basi bila shaka watarudishwa (adhabuni). Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa (na Mwenyezi Mungu). Na tumemuach...

HISTORIA YA NABII SULEIMAAN

Image
HISTORIA YA NABII SULEIMAAN Nabii Suleyman (AS) ni mtoto wa Nabii Daud (AS) Manabii hawa walijaaliwa na Mwenyeezi Mungu ilimu kubwa na Hikma. Walikuwa katika waja wema, wingi wa kushukuru kwa wanachoneemeshwa,wanyenyekevu na wepesi kurudi kwa mola wanapokosea,walijaaliwa ufalme ambao haukuwahi kuonekana toka dunia ianze hadi dunia itaisha.Ufalme wao ni ruzuku itokanao kwa muumba mbingu na Ardhi na ziliomo ndani.Na katika Manabii walojaaliwa kuzaa mtoto kwa kupewa Daraja ya Unabii ni Suleyman (AS)Na wengine walobahatika na hili ni Yahya (AS) babake ni Zakariya (AS).Na Ismael na nduguye Ishaq walizaliwa na  Ebrahim (AS)Baba wa waumini wote.  Mwenyeezi mungu anasema katika Surat Nnaml Aya 15. .Na hakika tuliwapa Daudi na Sulaiman ilimu, na wakasema: Alhamdu Lillahi, Kuhimidiwa kote ni kwa Mwenyezi Mungu aliye tufadhilisha kuliko wengi katika waja wake Waumini. Nabii Suleiman (AS)  Qur’an imelitaja jina lake katika aya zipatazo 16.  Suleiman (AS) alirithishwa kiti cha uf...

HISTORIA YA NABII DAUD

Image
HISTORIA YA NABII DAUD Nabii Daudi(a.s) aliishi Bait-Ul-Lahm karibu na mji wa Jerusalem zaidi ya miaka 200 baada ya Mtume Musa(a.s).  Nasaba yake inatokea kwa Mtume  Ya‘aquub(a.s). Pamoja na kuwa Mtume wa  Allah(s.w), Daudi alikuwa pia mfalme wa Mayahudi (Bani Israil). Katika jamii za jahiliyah nasaba ya mtu na uwezo wake wa kiuchumi ilikuwa ni vigezo muhimu katika kuteua kiongozi. Mayahudi kwa kuyatupa mafundisho ya Mitume wao na kwa ukaidi wao walivitilia mkazo vigezo hivi vile vile.  Kwa hiyo alipoteuliwa Twaluti kuwa kiongozi wao, wakaona hafai kwa kuleta hoja ya mali. Hata hivyo, hoja hiyo inavunjwa na elimu na siha nzuri. Uislamu unasisitiza umuhimu wa kuiboresha akili kwa elimu na kiwiliwili kwa siha nzuri. Katika Uislamu mtu hapewi uongozi kwa sababu ya nasaba au uwezo wake wa kiuchumi bali kwa elimu na UchaMungu wake.  Twaluti baada ya kupewa uongozi aliyaongoza majeshi ya Mayahudi kupambana na Jaluti na majeshi yake. Kundi kubwa katika Mayahudi liliasi...

KISA CHA NABII MUSSA

Image
KISA CHA NABII MUSSA Jina lake kamili ni Musa bin Umraan bin Wahib bin Laawy bin Yaakub bin Ishaaq bin Ibrahim (AS). Pia inasemekana kuwa ni Musa bin Umraan bin Yashar bin Faahib bin Laawy bin---. Mama yake jina lake Yuhab (pia inasemeka jina lake ni Afahiyah) ambae vile vile ni mama yake Harun (AS). Bani Israiyl waliishi huko Misri kutokea wakati wa Yusuf (AS). Na hawa Bani Israiyl wanatokana na Yaakub (AS), ambae akijulikana kwa jina la Israiyl. Kama tulivyoona katika hadithi ya Yusuf (AS), aliwachukuwa wazee wake pamoja na ndugu zake kutoka Falastini wakahamia Misri na kaishi huko. Wanasema waandikaji historia kuwa walipoingia Misri walikuwa watu thamanini na sita, wakazaliana na alipokuja Musa (AS) kutoka nao Misri walikuwa idadi yao laki sita.  Firauni (Mfalme) aliyehukumu wakati wa Yusuf (AS) alikuwa jina lake Rayyan bin Alwalid, na Firauni huyu alimuachilia Yusuf (AS) mambo mengi ya kuendesha nchi kwa vile Yusuf (AS) alivyoiokowa nchi katika njaa kubwa. Wakaiishi Bani Israiy...