Ramadhwaan Ni Mwezi Wa Du’aa Na Du’aa Hutakabaliwa

Ramadhwaan Ni Mwezi Wa Du’aa Na Du’aa Hutakabaliwa



Du’aa ni ‘ibaadah kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 عَنِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي قَوْلِهِ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) قَالَ: ((الدُّعَاءُ هُوَ الْعِبَادَةُ)) وَقَرَأَ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) إِلَى قَوْلِهِ: ((دَاخِرِينَ))

Amesimulia Nu’maan bin Bashiyr (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu kauli yake [Allaah Subhaanahu wa Ta’aalaa]: 

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ

((Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni))

Amesema: ((Du’aa ndio ‘ibaadah)) kisha akasoma: 

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ﴿٦٠﴾

Na Rabb wenu Amesema: Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari katika kuniabudu wataingia Jahanam wadhalilike.  [Ghaafir: 60] [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad – Hadiyth Hasan Swahiyh]

 Juu ya hivyo, du’aa ni ‘amali tukufu kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى):

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لَيْسَ شَيْءٌ أَكْرَمَ عَلَى اللَّهِ تَعَالَى مِنْ الدُّعَاءِ))  

Kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)    amesema: ((Hakuna kitu kitukufu mbele ya Allaah kama du’aa))  [Swahiyh Adab Al-Mufrad]

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ameiadhimisha ‘amali ya kuomba du’aa khasa katika mwezi wa Ramadhwaan kwa sababu zifuatazo:

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA NABII SULEIMAAN

The Story of Prophet Dhul Kifl

Full Story of the Prophet Ayyub