Ramadhwaan Ni Mwezi Wa Du’aa Na Du’aa Hutakabaliwa
Du’aa ni ‘ibaadah kama ilivyothibiti katika Hadiyth:
عَنِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي قَوْلِهِ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) قَالَ: ((الدُّعَاءُ هُوَ الْعِبَادَةُ)) وَقَرَأَ ((وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ)) إِلَى قَوْلِهِ: ((دَاخِرِينَ))
Amesimulia Nu’maan bin Bashiyr (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu kauli yake [Allaah Subhaanahu wa Ta’aalaa]:
وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ
((Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni))
Amesema: ((Du’aa ndio ‘ibaadah)) kisha akasoma:
وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ﴿٦٠﴾
Na Rabb wenu Amesema: Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari katika kuniabudu wataingia Jahanam wadhalilike. [Ghaafir: 60] [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad – Hadiyth Hasan Swahiyh]
Juu ya hivyo, du’aa ni ‘amali tukufu kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى):
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لَيْسَ شَيْءٌ أَكْرَمَ عَلَى اللَّهِ تَعَالَى مِنْ الدُّعَاءِ))
Kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakuna kitu kitukufu mbele ya Allaah kama du’aa)) [Swahiyh Adab Al-Mufrad]
Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ameiadhimisha ‘amali ya kuomba du’aa khasa katika mwezi wa Ramadhwaan kwa sababu zifuatazo:

Comments
Post a Comment