Hakuweza Kulipa Swawm Kwa Sababu Miaka Michache Alikuwa Anazaa Siku Za Ramadhwaan




Al-Lajnah Ad-Daaimah

SWALI:

Nini hukmu kuhusu mwanamke aliyekuwa akizaa siku za Ramadhwaan (kwa kutokea hivyo) muda wa miaka michache na hakuweza kulipa Swawm ya siku alizokuwa hakufunga?

JIBU:  

Inawajibika kwa mwanamke aliyejifungua katika mwezi wa Ramadhwaan kulipa siku alizokuwa hakuweza kufunga siku za mbele.

Na ikiwa hakulipa siku hizo bila sababu inayokubalika katika Shariy’ah ya Kiislamu hadi imeingia Ramadhwaan nyingine, basi inampasa  alishe maskini kwa idadi ya siku alizokuwa hakufunga na pia afunge Swaum za siku hizo. 

Lakini kama kuchelewa kulipa kulikuwa kwa sababu inayokubaliwa katika Shariy’ah ya Kiislamu basi inamtosha kuzilipa tu siku hizo.

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

[Fataawa Ramadhwaan - Mjalada 2, Ukurasa  588, Fatwa Namba 573;
Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah wal-Iftaa. - Fatwa Namba 9861]

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA NABII SULEIMAAN

The Story of Prophet Dhul Kifl

Full Story of the Prophet Ayyub