3 : Baada Ya Kufariki Dunia





Baada Ya Kufariki Dunia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)

Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifariki dunia: macho yalibubujika machozi, mioyo ilihuzunika, ulimwengu uliingia kiza, na waumini wakijilaumu wenyewe kwa mabadiliko yatakayotokea baadaye. Mwalimu aliyekuwa kipenzi cha waumini wote na aliyekuwa rehema kwao, alifariki dunia. Mtu anapompoteza aliyekuwa kipenzi na anayeheshimiwa sana, moyo wake unajaa kumbukumbu; alikuwa akikaa pale; alikuwa akisimama pale; alikuwa akisema na kufanya kadha, na kadha.


Watu wanapompoteza wampendaye, kwa kawaida hutafakari na kukumbukia maneno na misemo aliyoitamka. Na kama aliyekufa alichukuliwa kama kiigizo, wanakumbuka nasaha zake, hususa nasaha za mwisho, wakikazana kwa moyo wao wote kuzitekeleza. Wanarejea maneno yake na kuyapa uhai mpya kwa utendaji.

Kama mioyo yenu ilijeruhiwa na kifo cha Mtume wenu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), basi jibidiisheni kutekeleza nasaha zake za mwisho. Irbaad bin Saariyah (Radhiya Allaahu ‘anhu) alisimulia;

“Mjumbe wa Alah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoa khutbah yenye umbuji na hekima, khutbah ambayo ilisababisha macho kububujika machozi na mioyo kutetema. Tulisema, “Ewe Mjumbe wa Allaah! Inakuwa kama kkhutbah ya kuaga! Yeye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema, “Muogopeni Allaah, na lazima msikilize na muwatii (walio katika mamlaka), hata kama mtumwa wa Kihabeshi atafanywa kiongozi wenu. Yeyote atakayeishi baada yangu ataona migogoro; hivyo kilichopo juu yenu ni Sunnah zangu na Sunnah za Khalifah walioongozwa baada yangu; zuiweni (yaani Sunnah zangu….) kwa magego yenu.[1] Na jihadharini na muwe mbali na mambo yaliyo zaliwa, kwani kila uzushi ni upotevu”.[2]

Tulisema, “Ewe Mjumbe wa Allaah! Hii ni kama khutbah ya kuaga! (ya mwisho)  sasa unatuagiza nini?

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema, “Nimewaachieni ushahidi uliowazi, ambao usiku wake ni sawa na mchana wake. Hapana aendaye kombo baada yangu isipokuwa yule aliyekhasirika.


Yeyote atakayeishi baada yangu ataona migongano mingi; na juu yenu ni yale myajuayo kutokana na Sunnah yangu na Sunnah ya Khalifah waongofu: Iumeni (yaani Sunnah yangu….) kwa magego yenu. Mnawajibika kumtii mtumwa wa Kihabeshi. Kwa hakika, muumini ni sawa na ngamia Anif (ngamia aliyewekewa mbao katika pua yake, kutokana na kuhisi maumivu, anamtii mpandaji) popote anapoelekezwa, anakwenda.”[3]

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA NABII SULEIMAAN

The Story of Prophet Dhul Kifl

Full Story of the Prophet Ayyub