Dua ya kuingia nyumba au chumba ulichofikia
Huenda hatujui ni nani aliyekaa hapo awali au ni matukio gani yametokea katika chumba cha hoteli kabla ambayo yanaweza kuathiri kukaa kwetu. Kwa hakika inasaidia kujikinga na madhara yoyote kwa kusoma Dua ifuatayo kama ilivyotajwa katika Hadiyth iliyopokelewa na Khawlah binte Hakim As-Sulaimiyyah Mtume saw amesema:
A'uzu bikalimatillahit-tammati min syarri ma khalaq
Yeyote anayeingia mahali, kisha akaomba:
“Najikinga kwa Maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyokamilika kutokana na shari ya vilivyoumbwa,” hakuna kitakachomdhuru mpaka atoke mahali hapo. (Sahih Muslim)

Comments
Post a Comment