Posts

Showing posts from March, 2024

BAADHI YA VITHIBITISHO JUU YA UKWELI WA UISLAMU

Image
 BAADHI YA VITHIBITISHO JUU YA UKWELI WA UISLAMU Mwenyezi Mungu amempa nguvu Mtume wake wa mwisho Muhammad S.A.W kwa Miujiza mingi na Ushahidi mwingi ambao unathibithisha kuwa yeye ni mtume wa kweli alietumwa na Mungu. Vile vile Mwenyezi Mungu amekipa nguvu Kitabu chake alichokishusha mwisho, ambacho ni Qur’an tukufu, kwa Miujiza mingi ambayo inathibitisha kuwa Qur’an hii ni Maneno halisi ya Mungu, aliyoyafunua, na kwa hiyo Qur’an haijatungwa na mtu yeyote . Sura hii inajadili baaadhi ya ushahidi huo. (1) Miujiza ya Kisayansi ndani ya Qur’an Tukufu  Qur’an ni maneno halisi ya Mwenyezi Mungu, ambayo aliyashusha kwa Mtume wake Muhammad S.A.W kwa kupitia Malaika Jibril (Gabriel.). Qur’an ambayo ilihifadhiwa na Muhammad S.A.W naye akawasomea Qur’an hiyo wafuasi wake. Nao, kwa zamu, waliihifadhi, kuiandika, na kuipitia pamoja na Mtume Muhammad S.A.W.  Zaidi ya hayo Mtume Muhammad S.A.W aliipitia Qur’an pamoja na Malaika Jibril kila mwaka mara moja na katika mwaka wa mwi...

UTANGULIZI

UTANGULIZI App hii ni muongozo mfupi wa kuufahamu Uislamu. Nayo ina Sura tatu. Sura ya kwanza, ‘‘ Baadhi ya vithibitisho juu ya ukweli wa Uislam ,’’ Sura hiyo inajibu baadhi ya maswali muhimu ambayo watu wanayauliza: Je ni kweli kwamba Qur’an ni maneno halisi ya Mungu, yaliyofunuliwa toka kwake ? Je ni kweli kuwa Muhammad S.A.W ni Mtume alietumwa na Mungu?  Je ni kweli kuwa Uislamu ni Dini ya Mungu ? Katika sura hii, zimetajwa aina sita za ushahidi:   Miujiza ya kisayansi ndani ya Qur’an tukufu: Sehemu hii inazungumzia (kwa picha) baadhi ya hakika (facts) za uvumbuzi wa kisasa wa kisayansi zilizotajwa katika Qur’an tukufu, ambayo ilikwishafunuliwa karne kumi na nne zilizopita. Changamoto Kuu ya Kuunda Sura Moja kama Sura za Qur’an Tukufu: Katika Qur’an, Mungu amewapa changamoto watu wote watunge sura moja iliyo kama sura za Qur’an. Tangu kufunuliwa kwa Qur’an, karne kumi na nne zilizopita, mpaka leo, hakuna mtu aliyeweza kuifikia changamoto hii, ingawa sura ndogo sana ...