Posts

Showing posts from March, 2023

Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Katika Hadiyth Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

Image
Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Katika Hadiyth Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Zifuatazo ni baadhi ya fadhila zilizotajwa katika Hadiyth za kusoma na kuhifadhi Qur-aan.  1. Aliye Bora Kabisa Ni Ambaye Anajifunza Na Kuifundisha Qur-aan: عن عثمانَ بن عفانَ رضي الله عنه أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قالَ: ((خَيرُكُم مَنْ تعَلَّمَ القُرآنَ وعَلَّمَه)) صحيح البخاريِّ Imepokelewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mbora wenu ni yule mwenye kujifunza Qur-aan kisha akaifundisha)) [Al-Bukhaariy]  2. Anayeisoma Kwa Mashaka Hupata Thawabu Mara Mbili: عَنْ عَائِشَةَ رضي الله عنها قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((الْمَاهِرُ بِالْقُرْآنِ مَعَ السَّفَرَةِ الْكِرَامِ الْبَرَرَةِ، وَالَّذِي يَقْرَأُ الْقُرْآنَ وَيَتَتَعْتَعُ فِيهِ، وَهُوَ عَلَيْهِ شَاقٌّ لَهُ أَجْرَانِ)) البخاري ومسلم Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah...

Dua'a ya kuvaa nguo mpya

Image
SIKILIZA DUA'A Ewe Mwenyezi Mungu sifa njema ni zako, wewe ndiye uliyenivisha, nakuomba kheri ya nguo hii, na kheri ya kila ambacho nguo hii imetengenezewa, na najilinda kwako kutokana na shari yake, na shari ambayo nguo hii imetengenezewa.

Dua ya kuvaa nguo

Image
ISIKILIZE HAPA Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambae amenivisha nguo hii, na kuniruzuku pasina uwezo kutoka kwangu wala nguvu. (Waitoa Ahlu Ssunani isipokuwa Nnasai: Abuu Daud, namba 4023, na Tirmidhy, namba 3458, na Ibni Maajah, namba 3285, na akaifanya nzuri Albaany katika Ir'waai Al-ghaliil, 47/7)

Nyiradi za asubuhi na jioni sehemu ya pili

Image
 1. Bonyeza kusikiliza {Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu}. (Suratul-Baqarah: 255). Mwenye kuisoma (Ayatul-Kursiy) pindi anapoamka atalindwa kutokana na majini mpaka jioni, atakaeisoma jioni atalindwa nayo mpaka asubuhi. 2. Bonyeza Kusikiliza  Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. {Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee* Mwenyezi Mungu Mkusudiwa* Hakuzaa wala hakuzaliwa* Wala hana anaye fanana naye hata mmoja}. Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu. {Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko* Na shari ...

Nyiradi za wakati wa kulala

Image
1. Bonyeza kusikiliza Alikuwa Mtume (s.a.w) akitaka kulala usiku akivikusanya viganja vyake vya mikono kisha akivipulizia na akivisomea Suratul-Ikhlas, na Suratul-Falaq, na Suratu Nnas, kisha akijipangusa kwa hivyo viganja vyake katika mwili wake kiasi anachoweza, akianza kichwani na usoni na mbele. (Akifanya hivo mara tatu). 2. Bonyeza Kusikiliza   Mtume (s.a.w) amesema: (Ukitaka kulala soma Ayatul-Kursiy mpaka umalize kwani Mwenyezi Mungu ataendelea kukuhifadhi, wala hakukaribii shetani mpaka asubuhi. {Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu}. (Suratul-Baqra...

Duaa mbalimbali za Qunoot

Image
1. Bonyeza  kusikiliza "Ewe Mwenyezi Mungu, niongoze pamoja na uliowaongoza, na unipe afya njema pamoja na uliowapa afya njema, na nifanye kuwa ni mpenzi wako pamoja na uliowafanya wapenzi, na nibariki katika ulichonipa, na nikinge na shari ya ulilolihukumu, kwani Wewe unahukumu wala huhukumiwi, hakika hadhaliliki uliyemfanya mpenzi (wala hatukuki uliyemfanya adui) Umetakasika Ewe Mola wetu na Umetukuka." 2. Bonyeza Kusikiliza "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako, na kwa msamaha wako kutokana na adhabu yako, na najilinda kwako kutokana na Wewe, mimi siwezi kudhibiti sifa zako, Wewe ni kama ulivyojisifu Mwenyewe." 3. Bonyeza Kusikiliza "Ewe Mwenyezi Mungu, Wewe tu ndiye tunaekuabudu, na kwako tunasali na tunasujudu, na kwako tunakimbilia na tunakutumikia, tunataraji rehema yako, na tunaogopa adhabu yako, kwani adhabu yako hakuna shaka kuwa makafiri itawafikia. Ewe Mwenyezi Mungu hakika sisi tunakutaka msaada, na tun...

Sayyidul Istighfaar Du’aa Bora Kabisa Ya Kuomba Maghfirah Na Fadhila Za Kuomba Tawbah

Image
BONYEZA HAPA KUSIKILIZA DUA HII Du’aa hii imeitwa Sayyidul-Istighfaar (Du’aa bora au adhimu kabisa ya kuomba maghfirah kuliko istighfaar nyenginezo) kwa sababu imekusanya kukiri Tawhiyd Al-Uluwhiyyah (‘ibaadah), Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah (Uola), kukiri dhambi za mja, kunyenyekea mja kwa Rabb wake, kutambua neemah za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amghufurie madhambi yote.    اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك، وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت، أَعـوذُبِكَ مِنْ شَـرِّ ما صَنَـعْت، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ . Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana ‘abduka wa anaa ‘alaa ‘ah-dika wawa’-dika mastatwa’-tu, a’uwdhu bika min sharri maa swana’-tu, abuw-u Laka bini’-matika ‘alayya wa abuw-u bidhanbiy, faghfir-liy fainnahu laa yaghfirudh dhunuwba illaa Anta Ee Allaah, Wewe ...

Swalah Na Du’aa Zipi Za Kusoma Unapotaka Kutubu?

Image
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.  Hakika bin adam ni mwenye kukosa, na hakika bin adam mwenye aqil ni yule anapoona amekosa basi anamrudia Mola wake na kumuomba Maghfirah. Ikiwa ni miongoni mwa hao basi hilo linalokupasa  kumshukuru Allaah (Subhaanahu Wa Ta'alaa) kwa Kukuzindua ukatambua kuwa uko makosani kabla ya adhabu Yake au mauti kukufika. Yote hayo ni neema kutoka kwa Mola wako unapasa umshukuru sana kila wakati.  Kuomba Maghfirah unaweza kuswali Rakaa mbili tu kwa nia moyoni ya kuomba Tawbah kwa Mola wako kama utakavyoona dalili katika mada za Tawbah tunazokuwekea viungo vyake chini.  Ama du’aa, ziko mbali mbali ambazo hata Mitume waliomba walipokuwa wakifanya makosa au katika kawaida ya kumdhukuru Allaah, pamoja na adhkaar mbali mbali alizotufun...

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

Image
Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah Kila amali njema atendayo Muislamu inalipwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) mara kumi yake, isipokuwa Swawm  ambayo malipo yake ni makhsusi kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama ilivyothibiti katika Hadiyth: عنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ يُضَاعَفُ الْحَسَنَةُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا إِلَى سَبْعمِائَة ضِعْفٍ قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ إِلَّا الصَّوْمَ فَإِنَّهُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ))    Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu): ((Kila ‘amali njema ya mwana Aadam inalipwa mara kumi na inaongezewa thawabu kutoka kumi hadi mia saba, na Allaah (‘Azza wa Jalla) Anasema: Isipokuwa Swawm, kwani hiyo ni kwa ajili Yangu na Mimi Ndiye Nitakayemlipa]  [Muslim na Ahmad] Juu ya hivyo Swawm ina fadhila tele adhimu kama ifuatavyo: عَنْ أَبي ذَرٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ ع...